Home » » WANASIASA WANAOKATAZA WANANCHI KUTOA MAONI YA KATIBA MPYA WAONYWA

WANASIASA WANAOKATAZA WANANCHI KUTOA MAONI YA KATIBA MPYA WAONYWA

Na Mwandishi Wetu, Kigoma Yetu

Viongozi wa Vyama vya Siasa Mkoani Kigoma wameonywa kuacha kuwakataza wananchi wasiende kwenye mikutano ya kutoa maoni yao juu ya mchakato wa katiba mpya.

Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kigoma Khamis Bitese  alipokuwa akizungumza na wandishi wa habari Mkoani hapo, ambapo alisema kutokana na mchakato wa utoaji wa maoni wanasiasa wengi wamekuwa wapotoshaji wa jamii, kwa kuwapotosha wanajamii wasiweze kutumia fursa hiyo ili hali wao wanaenda kwenye mikutano mbalimbali ambayo hutolewa na baadhi ya asasi zilizopo.

Bitese aliwataka wananchi kutambua haki zao pasipo kufuata utashi wa vyama vya siasa kwani kwa kufanya hivyo ni kujidhulumu haki zao wenyewe.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Miriam Mbaga alisema wamejipanga vyema kuhamasisha jamii kutoa maoni yao na tayari wameshatoa katiba 18 kwa baadhi ya madiwani ikiwa na chachu ya kuwaelimisha wakazi wa kata zao.

Pia alizitaka asasi zisizo za kiserikali kutumia nafasi zao kuelimisha wakazi wa Mkoa huo. Tume ya kukusanya maoni itaanza kazi zake Mkoani Kigoma kuanzia Septemba 13-28 mwaka huu.

Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa