Home » » MISSENYI YATOA MIKOPO MIL 60

MISSENYI YATOA MIKOPO MIL 60

Halmashauri ya wilaya ya Missenyi mkoani Kagera imetoa mikopo ya zaidi ya shilingi milioni 60.1 kwa vikundi mbalimbali vya wanawake na vijana katika kipindi cha miaka sita iliyopita.

Taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa halmashauri hiyo Elzaberth Kitundu imesema kuwa mikopo hiyo imetolewa kuanzia mwaka wa fedha 2007/2008 hadi 2012/2013.

Kitundu amesema kuwa katika kipindi hicho vikundi vya akina mama vilipatiwa mikopo ya zaidi ya shilingi milioni 40.8 ambapo  vikundi vya vijana vilipatiwa mikopo ya zaidi ya shilingi milioni 19.3.

Amesema kuwa lengo la halmashauri hiyo kuviwezesha vikundi vya wanawake na vijana kwa kuwapatia mikopo  ni kutaka  kuinua mitaji yao,  na kuwa hali ya marejesho kwa vijana sio mbaya isipokuwa kwa upande wa wanawake ndio wanarejesha kwa kusuasua.

Amesema kuwa katika kuhakikisha vikundi hivyo vinakuwa endelevu, wamekuwa wakiwashauri wanachama wake kuanzisha vyama vya akiba na mikopo (SACCOS) na kuwa katika wilaya hiyo hadi sasa kuna vyama vya ushirika 73, vikiwamo vya mazao 28, Saccos 36 ambapo vyama tisa ni vya mchanganyiko.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa