Home » » Kilaini atoa neno la 2014

Kilaini atoa neno la 2014

Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki nchini, Jimbo Kuu la Bukoba, mkoani Kagera, Method Kilaini ametoa wito kwa Watanzania kupiga vita viashiria vya uvunjifu wa amani.

Alisema mwaka 2014, Watanzania wote wanapaswa kuilinda amani iliyopo hasa kipindi hiki cha mchakato wa kupata Katiba Mpya kwani wapo baadhi ya watu wachache wanaoonesha
viashiri vya uvunjifu wa amani.

Askofu Kilaini aliyasema hayo jana wakati akizungumza na Majira ili kupata maoni kwa Watanzania ambao leo saa sita usiku, watauanza mwaka mpya wa 2014.

"Amani tuliyonayo hatupaswi kuichezea hata kidogo, nchi nyingine wanaitafuta kwa muda mrefu na hawaipati hivyo tusiruhusu mtu yeyote aichezee amani yetu," alisema.

Aliwataka Watanzania kuendeleza umoja na mshikamano dhidi yao bila kujali dini, ukabila wala rangi

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa