Home » » Mwalimu jela miaka saba kwa kumkata kiganja mwanafuzi

Mwalimu jela miaka saba kwa kumkata kiganja mwanafuzi

Mwalimu wa Shule ya Sekondari Rwambai Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera, Alliamin Mtabuzi (25), amehukumiwa kifungo cha miaka saba jela baada ya kupatikana na kosa la kumkata kiganja cha mkono mwanafunzi wake wa kidato cha nne.
Mtabuzi alipatikana na kosa la kumsababishia ulemavu mwanafunzi huyo, Annocietha Theobart (16), kutokana na wivu wa mapenzi.

Mbali ya kifungo hicho, pia ameamriwa kumlipa mlalamikaji huyo fidia ya Shilingi milioni tano.

Hukumu hiyo ilitolewa na Novemba 27, mwaka huu na Jaji Peragia Hadai wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba.

Akitoa hukumu hiyo, Jaji Hadai alisema itakuwa fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

Awali, Wakili wa Serikali, Safina Simba, alidai  kuwa mshatakiwa alitenda kosa hilo mwaka 2008 katika kijiji cha Rwambai wilayani Karagwe nyumbani kwa mlalamikaji kwa madai kwamba mwanafuzi huyo alikuwa na mchumba mwingine.

Baada ya kufika nyumbani hapo, mshtakiwa alianza kumshabulia mama mzazi wa mlalamkaji kabla ya kumshambulia malalamikaji kwa panga na kumkata kiganja cha mkono wa kulia pamoja na kidole cha mkono wa kushoto.

Hata hivyo, mwanafunzi huyo katika ushahidi wake alidai mahakamani hapo kuwa hakuwa na makubaliano ya uchumba na mshtakiwa.

Naye wakili wa utetezi, Alliamini Chamani, alidai kuwa mahakama inastahili kumpunguzia adhabu mshtakiwa kwa kuzingatia kuwa alikuwa mchumba wa mlalamkaji kwa makubaliano angemuoa baada ya kumaliza shule.

Alidai kuwa mshtakiwa huyo alikuwa akimgharimia mlalamikaji karo ya shule na mahitaji mengine yote muhimu hivyo alikasirishwa baada ya kubaini  alikuwa na mchumba mwingine.

Hata hivyo, Mahakama iliotupilia mbali utetezi huo na kumpa mshtakiwa adhabu ya kifungo cha miaka saba pamoja na kumlipa mlalamikaji fidia ya Sh.milioni 5.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa