Home » » HALI YA HEWA KAGERA YAVUTA WAWEKEZAJI

HALI YA HEWA KAGERA YAVUTA WAWEKEZAJI

HALI ya hewa na mandhari ya Mkoa wa Kagera  imeelezwa  kuwa ni kivutio kwa wawekezaji katika sekta mbalimbali zikiwemo za kilimo, ufugaji na viwanda.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa juzi na Balozi wa China nchini Tanzania, Dk. Lu Youging katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Fabian Massawe kilichokuwa kikielezea fursa za uwekezaji  mkoani hapo.
Dk. Youging  alisema Mkoa wa Kagera una ardhi nzuri  yenye rutuba inayofaa kwa kilimo licha ya kuwepo kwa vyanzo mbalimbali vya maji ambavyo husaidia katika kilimo cha umwagiliaji bila kusubiri kipindi cha masika.
Alisema pia mkoa wa Kagera una sehemu nzuri ya utalii ambayo ni fursa nzuri ya kuendeleza na kuinua uchumi wa mkoa.
Alisema pamoja na kuwepo kwa fursa nyingi za uwekezaji mkoani hapo, bado soko si zuri  na kueleza kuwa soko likiwa zuri wawekezaji zaidi watajitokeza.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa