Home » » ZAIDI YA MIL.500/- ZAHITAJIKA SHEREHE ZA MWENGE KGERA

ZAIDI YA MIL.500/- ZAHITAJIKA SHEREHE ZA MWENGE KGERA

Zaidi ya Mil. 500/- zahitajika sherehe za mwenge KageraMKUU wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Fabian Massawe, amesema zaidi ya sh milioni 500 zinahitajika kukamilisha sherehe za kuwasha mwenge kitaifa, Mei 2, mwaka huu.
Kanali Massawe aliwaomba wadau walioahidi kuchangia katika sherehe hiyo kukabidhi michango yao mapema ili maandalizi yaweze kukamilika.
Akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa hivi karibuni, Kanali Massawe alisema sherehe hizo zitafanyika katika Uwanja wa Kaitaba na mgeni rasmi atakuwa  Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilali.
Alisema wakati wa mbio za mwenge, miradi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii itazinduliwa ambapo kwa sasa wanaendelea kuorodhesha miradi hiyo katika kila wilaya.
Kanali Massawe alisema baada ya mwenge kuwashwa, mbio zake zitaanza katika Manispaa ya Bukoba na kumalizia Wilaya ya Biharamulo.
“Naishukuru sana serikali  kuona umuhimu wa mwenge wa uhuru  kuwashwa Kagera kwa lengo la kuchochea maendeleo ya wananchi,” alisema Massawe.
Alisema wananchi wanatakiwa kujitokeza kwa wiki kuupokea mwenge huo na kusema kuwa patakuwepo na michezo mbalimbali katika sherehe hizo.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa