Home » » Wafugaji wavamizi waonywa

Wafugaji wavamizi waonywa

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo, mkoani Kagera, Nassibu Mmbaya, ametoa onyo kwa wafugaji wanaovamia misitu wilayani hapa na kutaka waache mara moja tabia hiyo.
Mmbaya alitoa onyo hilo juzi alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Alisema wafugaji hao ambao wanavamia misitu wilayani hapa wanatoka sehemu mbalimbali  ikiwemo Geita, Kahama,  Bariadi pamoja na maeneo mengine nchini.
Alisema kadrii siku zinavyozidi kwenda misitu hiyo itazidi kupukutika kutokana na wafugaji hao kuongezeka.
"Wafugaji hawa wanaingia Biharamulo kwa lengo la kuishi, lakini cha kushangaza wamekuwa ni watu wa kuvamia  maeneo  ya misitu, ukiwemo ule wa Kasindaga.
“Hili jambo linasababisha uharibu wa misitu ikiwa ni pamoja na kutokea mmonyoko wa udongo," alisema mkurugenzi huyo.
Alisema ili kudhibiti uvamizi huo, tayari halmashauri yake imeshaanzisha operesheni maalumu ya kuwaondoa wafugaji hao katika maeneo yasiyoruhusiwa.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa