Home » » Umaskini chanzo cha vifo vya wajawazito

Umaskini chanzo cha vifo vya wajawazito

IMEELEZWA kuwa wajawazito wengi wanapoteza maisha wakati wa kujifungua kutokana na umaskini wa kipato.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Muuguzi Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo, mkoani Kagera, Revocatus Dominick, alipozungumza na Tanzania Daima Jumapili lilipomtembelea ofisini kwake.
Alisema, umbali wa vituo vya afya ni sababu inayochangia kwa kuwa wengi wao wanakosa fedha za usafiri wa kwenda kwenye vituo hivyo au hospitali.
“Umaskini unasababisha wanawake wengi kufariki dunia wakati wa kujifungua… watoto hufia tumboni mwa mama zao kwa vile wanachelewa kufika hospitalini,” alisema Dominick.
Awali aliwataka wanaume kuwasindikiza wake zao kliniki wakati wa ujauzito ili kwenda kupata ushauri na maelekezo kutoka kwa wataalamu wa afya wakiwa pamoja.
“Sababu nyingine ni uelewa mdogo wa jamii kuhusu elimu sahihi ya afya ya uzazi, ukarimu wa wahudumu, jambo linalochangia wajawazito wengi kutofika kwenye vituo vya afya,” alisema.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa