Home » » WAHAMIAJI 32 WAKAMATWA KAGERA

WAHAMIAJI 32 WAKAMATWA KAGERA

Wahamiaji haramu 32 raia wa Burundi wamekamatwa na idara ya uhamiaji mkoni Kagera wakidaiwa kuingia nchini kinyume na sheria.

Afisa uhamiaji mkoani Kagera,  George Kombe amesema kuwa wahamiaji hao walikamatwa jana kutokana baada ya kupata taarifa kutoka kwa  raia wema .

Kombe amesema kuwa wahamiaji hao haramu walikuwa wakisafirishwa kwa gari aina ya Hiace lenye namba T633 CPZ , na kuwa walipohojiwa baadhi yao walisema walikuwa wakielekea nchini Burundi huku wengine wakidai walikuwa wakielekea kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu mkoani Kigoma.

Amesema kuwa utaratibu wa kuwasafirisha wote hadi mpakani mwa nchi yao umekamilika na kuahidi kumchukulia hatua za kisheria dereva wa gari hilo  kutokana na kuwasaidia wahamiaji haramu hao kuingia nchini kinyume na sheria.

Baadhi ya wahamiaji hao walipohojiwa na vyombo vya habari wamesema  kuwa wametoroka kutoka kambi ya wakimbizi ya Nyakivary nchini Uganda kutokana na hali ya maisha kuwa ngumu.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa