Home » » TCRS yatoa vifaa vya zaidi ya milioni 60 kwa waathirika wa tetemeko Kagera.

TCRS yatoa vifaa vya zaidi ya milioni 60 kwa waathirika wa tetemeko Kagera.



Na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Bukoba.
Shirika la Kiristo la Kuhudumia Wakimbizi Tanganyika (TCRS) limechangia vifaa vyenye jumla ya Sh. milioni 60.92 ikiwa ni mchango wao wa kuwafuta machozi wanakagera baada ya kuathiriwa na tetemeko la ardhi.

Katika kuhakikisha hali za wananchi na ttaasisi za kutolea huduma za kijamii  zinaimarika na kurudi kwenye hali ya kawaida, wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi bado michango yao inahitajika.

Akikabidhi mchango huo, Mratibu wa Miradi inayoendeshwa na TCRS Oscar Rutenge pamoja na Jasmine Gwamsy wametaja mchanganuo wa msaada huo kuwa ni pamoja na blanketi, 1680, mashuka 840, ndoo za kutumia 840, nguo za kutumia kwawanawake, wanaume na watoto box 50, sabuni katoni 1680 pamoja na vifaa vingine 2250.

Akipokea msaada huo Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu amemelishukuru shirika hilo kwa mchango wao huo kwani ni wa thamani hasa baada ya tetemeko hilo kuwaaathiri wananchi wa mkoa huo.

Aidha, Meja Jenerali Mstaafu Kijuu amewakaribisha na kuwataka wadau wengine waguswe kwa namna ya kipekee na waendelee kutoa michango yao waweze kuwasaidia wananchi na kurudisha hali yao  na kuendelea na shughuli zao za kijamii na kimaendeleo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa