Home » » 13 KORTINI KWA KUZUIA SENSA

13 KORTINI KWA KUZUIA SENSA



na Mbeki Mbeki, Bukoba
WATU 13 wamefikishwa mahakamani mkoani Kagera kutokana na kuingilia shughuli za Sensa ya Watu na Makazi na kuzuia isifanyike.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Fabian Massawe, alipokuwa akitoa taarifa ya Mkoa kwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, katika ziara yake ya kiserikali mkoani Kagera.
Alisema watu hao wamefikishwa mahakamani kwa nyakati tofauti kutokana na vitendo vyao vya kukataa kuhesabiwa na baadhi yao kuhamasisha watu wengine kutoshiriki sensa katika wilaya mbalimbali za mkoa huo.
Alisema watu hao walitoka katika Wilaya ya Misenyi (5), Manispaa ya Bukoba (5), Kyerwa (1) na Muleba (1).
Aidha, alimhakikishia Waziri Sitta kuwa taarifa zote zitakazokusanywa katika shughuli hiyo zitakuwa siri kwa mujibu wa sheria ya takwimu ya mwaka 2012 na zitatumika kwa shughuli za kitakwimu pekee.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa