Home » » Halmashauri yalalamikiwa

Halmashauri yalalamikiwa

Karagwe. Baadhi ya abiria Mji Mdogo wa Kayanga na wamiliki wa daladala, wamelalamikia uongozi wa Halmashauri ya Karagwe kushindwa kutengeneza miundombinu ya stendi ya wilaya miaka 50 iliyopita tangu wilaya kuanzishwa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya abiria walionyesha kukerwa na magari kujipanga kandokando barabara kutokana na ubovu wa stendi.
Selian Katabazi alisema utaratibu unaotumiwa wa kuegesha magari kandokando ya barabara, ni hatari kwa maisha ya watu.
Katabazi alisema inashangaza kuona makao makuu ya wilaya ambayo imeanza miaka 50 iliyopita, ikiwa imeongozwa na wakuu wa wilaya 21 na wakurugenzi 14 haina miundombinu ya kuridhisha.
Nao wamiliki wa daladala, walisikitishwa na halmashauri kuendelea kukusanya ushuru katika stendi ambayo haikidhi vigezo. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe, Bosco Ndunguru akijibu swali la Diwani wa Kata ya Kayanga, Adventina Kahatano (CUF) alipotaka kujua hatua ya makao makuu ya wilaya kutokuwa na stendi, alisema itapangiwa bajeti mwaka ujao wa fedha na kukukiri kuwa haikuwekwa kwenye vipaumbele vya bajeti mwaka huu.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa