Home » » TAARIFA KAMILI : MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI AFANYA KIKAO KIZITO BUKOBA LEO.CHAMFUKUZISHA KAZI MEYA NA WENGINE KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA.

TAARIFA KAMILI : MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI AFANYA KIKAO KIZITO BUKOBA LEO.CHAMFUKUZISHA KAZI MEYA NA WENGINE KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA.




Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Ludovick Utouh akitoa taarifa ya ukaguzi maalum leo Bukoba. Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri akiendelea kutoa Maelezo ya Serikali. Kuhusu Suruhisho hilo ambapo yamebainika Makosa ya Meya Anatory kufanya makubaliano bila idhini ya Madiwani na Taratibu za serikali, Basi ajipime Mwenyewe na Kujiuzulu mara moja kwa Maslahi ya Manispaa ya Bukoba. Mkuu wa mkoa wa Kagera Mh.Fabian Massawe akimkaribisha mgeni Rasmi leo kwenye kikao hicho cha kukamilisha Ukaguzi Maalum" Exit Meeting"  Cha mdhibiti na mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali leo Januari 17.2014 Mjini Bukoba ambapo kikao hicho kilianza mapema saa 5 Asubuhi.
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye kikao hicho kizito kilichofanyika leo mjini Bukoba na kupelekea Meya Anatory Amani kujiuzulu kufuatia ubadhirifu wa fedha uliobainika.
== SOMA TAARIFA YA CAG HAPA CHINI. ===== =====  ======= TAARIFA YA CAG
Waziri mkuu alituomba tufanye ukaguzi maalum,
Mwaka 2013 tulifika bukoba na kufanya kikao cha kwanza na wadau.
Katika kikao hicho nilitoa maombi ambayo mliyafuata nawashukuru,madiwani na wananchi walitusaidia saan

Natoa taadhari kwamba tulikuwa na adidu za rejea ambazo ndizo tulizofuata,tulipokea mombi ya wananchi wengi lakini hayakuwepo katika adidu za rejea,hatukuyafanyia kazi

Kilichobainika
Tunapohitaji maendeleo,tunafanya vitu kwa nia njema bila kufuata taratibu


Kuhusu uwekezaji wenye mashaka kwenye kituo cha kuosha magari,zabuni haikuwa shindanishi  ni kiyume na taratibu cha taribu anataja kifungu kilichokiukwa
Waliosaini ni Khamis kaputa na anatory amani huku wakijua ilikuwa ni makosa kufanya hivyo bila idhjini ya kikao cha madiwani,pia kamupuni husika ya ASEC ilikuwa haijasajiliwa na BRELA. hailipi kodi TRA


2.Issue ya Viwanja

kati ya wananchi 800 waliotakiwa kugawiwa viwanja ni 300 waliogawawia kutokana na migogo ya viwanja kimila.


Manispaa ilingia makubaliano na UTT kupima viwanja elfu 5 kwa kuggawana faida ya asilimia 50 kwa 50 baina ya UTT manispaa ilisainiwa na kaimu meya ngalinda bila kupata idhini ya baraza la madiwani

Pia walikopa fedha kutoka UTT bila kupata ridhaa ya waziri mwenye thamana.

3.Issue ya matengenzo ya barabara mpya


Manispaa ya bukoba iliingia mkataba na mkandarsai aitwaye KAJUNA INVESTMENT mkataba ulikuwa wa sh 138 milioni alilipwa fedha za dharula amabzo hazikuwa na nyaraka hivyo malipo ya mkandarasi huyu yaliongezwea hadi kufikia sh sh 227 kwa kutumia barua iliyosainwa na tofauti na hali ya awali.haikuwapa idhini ya mkandarsi wa serikali na kinyume na kanuni za manunuzi ya umma.anasoma kifungu kilichokiukwa

 
4.issue ya Ujenzi wa soku kuu

Utaratibu wa kutaka kujenga soko kuu la bukoba haikupata idhini ya madiwani ya kumlipa mkandarasi mshauri OGM milioni 789 huku pia akawaita madiwani na kuwaeleza kuwa mkandarasi anahitaji jumla la miliini 590 mlioni. Mmojawapo wa madiwani mhg lunagisa alikataa pale pale kwenye kikao.

5.Issue ya kuhamisha wafanyabisha wa bukoba

Mh Meya anatory aman aliomba mkopo kwa kazi hiyo bila kibali cha madiwani na mawaziri.mkpo huo hata hivyo haukupoatika
6.Mkandaasi wa OGM hakuwa kwenye orodha ya walioomba zabuni ya kufanya kazi ya ukandarasi ushauri wa kufanya kazi katika ujenzi wa soko kuu lakini alionekana kwenye rodha baadye ya waliolipwa .Wakandarasi wote waliolipwa fedha hizo walikuwa hawalipi kodi TRA-hivyo TRA ina haki ya kuwadaiu hizo kodi.


7.Ujenzi wa stendi kuu ya bukoba

Mradi huu hakutengezwa kwenye gazeti la sertikali lakini walipata mkandarasi na kumlipa fedha za kazi hiyo kinyume na taratibu za serikali.gazeti lilotangaza tenda hiyo halikupatikana.pia timu ya ukaguzi ilitembelea eneo al kazi na kubaini kuwa mkandarasi alilipwa fedha nyhingi tofauti na kazi aliyoifanya


9.Mradi wa maji

Kila kata iliyopangwa kuwekwa mradi wa maji ilitakiwa kuchangia asilimia 2 hivyo kata anakotoka meya ilitiumiza kigezo na kupata huduma hiyo.fedha za kata zilitolewa na meya kwa kata yake.hivyo kitendo cha kata ya meya kupata huduma hakuwa na tatizo.Tuhuma hizi kuwa meya alitoa huduma kwa kata yakle ni uongo.
10.Issue ya uuzwaji viwanja vya wazi.
Mkataba wa kununua kiwanja kinacholalamikiwa hakufuata taratibu za ununuzi
Ni katika bweni la sekondari ya PEACE inayomilikiwa na Meya.Tunapendekeza kuundwa kwa trimu maalum kuchunguza tuhuma hizi kwani katika eneo hili hatukufikia mwisho




11.Ujenzi wa barabara kwa lami kwenye kata ya meya toafuti na fedha zilizoombwa

Manispaa iliomba milioni 30 kukaqrabati barabarab hiyo akini TAMISEMI ilitao milioni 300 na walihoji TAMISEMI walisema hilo ni la kawaida hivyo tuhuma hizo ni UONGO


12.Mradi wa Ujenzi wa Bwawa 

Hakuwahi kujadiliwa na baraza la madiwani,ulikuwa ni mradi wa wajanja tu



13.Issue ya wafganyabishara soko kuu kutolipa kodi

Manispaa Imekosa mapato sh milioni 256 zimpotea kutokana na chanzo hizo cha wafanyabishara wa soko kuu kutolipa kodi kutokana na mgogoro unaondelea


14.Issue ya matumizi ya gari Sm 4663

Gari hili limekuwa likiegeshwa kwa ofisi ya redio kasibante ya kagasheki.kumbukumbu za TRA zinaonesha kuwa ni mali ya halmashauri lakini alipohojiwa kagasheki alidai kuwa alinunua kwa fedha zake. Lakini halmshauri haina kumbukubu zozote juu ya gari hilo



Tunapendekeza alilrejeshwe kwenye halmshauri kama ataona ni manufaa kwa wananchi lakini kama haitawezekana basi gari hilo libadilishiwe usajhili ili lionekbnane ni la kiraia


15.Uteuzi wa wakala wenye upendeleo kwenye ushuru wa basi

Zabubi ya aliyepata rufaa ilitenguliwa kwani haikuwa imesajiliwa na mamlaka husika
Alibadilisha jina na kuomba tena kasha kupata,muombaji aliyeomba kwa tozo ya juu alinyimwa.





Manispaa ilifanya upendeleo na kukosa sh million 46 kwa mwaka




16:Issue ya posho kwa madiwani katika safari ya mafunzo nje ya wilaya.

Madiwani wawili walitakiwa kulipwa sh laki 4 kila mmoja kwa safari hawakusafiri lakini fedha hizo hazikurudishwa kwa manispaa na kukatiwa risiti,.hazionekjani zilipo






17.Issue ya vibanda vya maduka

Ukaguzi hakudhibitisha kuwepo tatizo la katika dai hili kwani nyaraka zinaonesha kutokuwepo tatizo.bali inashauri kuwepo kwa mkanganyiko na wapangaji wake





18.Issue ya deni katika uwanja wa mpira kaitaba.

Uwanja ulikarabatiwa na kiwanda cha sukari kagera kwa madai ya kurejeshewa fedha zake.sehemu ya fedha hazijarudishwa.Tume inapendekeza kufanya muafaka na kiwana au itafute fedha za kulipa deni





19.Kutowajibika ipasavyo kwa ukaguzi wa ndani.

Kipo kwa ajili ya kushauri na kuziba mianya ya matumizi mabaya ya fedha.
Aliyekuwepo amehojiwa juu ya miradi hiyo na kwamba halikuwa hajui lolote na hakuweza kumshauri mkurugenzi ipasavyo





20.Mteuzi katika bodi ya maji.upendeleo kwa mmoja wa madiwani

Waziri mwenye thamana aliteuwa



Hitimisho.

Hatukuweka chumvi,tuliyosema ndiyo ukweli tupu
Namshukuru waziri mkuu kwa kunipa kazi hii ya kukaguzi katika manispaa





Utaratibu wa uwasilisahji wa ripoti maalum tutaipeleka kwa aliyeomba ukaguzi huu.

ASANTENI AMEMALIZA





Mwanry anaongea sasa

Kwa niaba ya waziri mkuu naomba nitoa taarifa hii kama ifuatavyo





Maelekezo ya waziri mkuu.

Makosa ya meya anatory kufanya makubaliano bila idhini ya madiwani na taratibu za serikali basi ajipimemwenyewe na kujiuzuru kwa maslahi ya manispaa ya bukoba.





Akikataa basi madiwani wamuondoe





Watumishi wa manispaa wachukuliwe hatua

Bw Khamis kaputa avuliwe madaraka
Mhandisi,mweka hazina nk wapoteze vyeoi vyao





Wakandarasi wote waliopata fedha bila taratibu wazirejeshwe

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa