Home » » KAMPENI TOKOMEZA MNYAUKO KUWAFUNGA WAKULIMA WAKAIDI

KAMPENI TOKOMEZA MNYAUKO KUWAFUNGA WAKULIMA WAKAIDI

Kyerwa. Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu Fabian Massawe ametangaza kuanzisha jitihada za kudhibiti ugonjwa wa mnyauko unaoathiri migomba unaoenea kwa kasi Wilaya ya Kyerwa, Mkoa wa Kagera,
Hatua hiyo ilitangazwa na Ofisa Kilimo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa juzi, Stella Ndea na kwamba inatarajia kuanza wiki ijayo.
Alikuwa akizungumza na wakulima wa vijiji vya Rutunguru na Kihanga, wilayani Kyerwa.
Ndea alisema tayari sheria ndogondogo zimetungwa kudhibiti watu watakaoshindwa kufuata ushauri unaotolewa na wataalamu wa kilimo, ambao ni kukata migomba ambayo iimeathirika.
Ndea alisema licha ya sheria hizo, ofisi ya mkuu wa mkoa imejiandaa kuendesha Operesheni Tokomeza Mnyauko itakayohusisha wilaya zote za mkoa na itahitimishwa Juni mwaka huu.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa